Saturday, June 16, 2012

CHELSEA KUSAJILI MKENYA!!!

Chelsea imetwajwa kuwa inaongoza foleni ya timu zinazofukuzia kumsajili mwana kandanda Victor Wanyama anatokea nchini Kenya .Mwanasoka huyo anaekipiga katika timu ya Celtic ya Scotland kwa mujibu wa msemaji wake ambae pia ni (Agent) wake , inasemekana anatafuta timu mpya ya kuchezea kwa ajili ya msimu ujao wa ligi.


Kocha wa Chelsea  RDM ambaye amekabidhiwa usukani rasmi siku kadhaa zilizopita wiki hii  kwa mkataba wa miaka miwili, anadaiwa kusaka kiungo mwenye nguvu na ujuzi wa kuiendesha timu pale kati na Victor anaonekana ni mmoja kati ya wanaofikiriwa kuja kuziba pengo la Essien anaeonekana kupungua kwa kiwango chake cha uchezaji tangu arudi uwanjani na huku rekodi yake ya kuumia umia kila mara ikiongezeka.

Agent wa mchezaji huyo bwana Rob Moore amedai mteja wake ana nia ya kucheza katika ligi kuu ya Uingereza na hatosita kama nafasi ikitoke haraka na yupo tayari hata sasa!
Habari za kuwepo sokoni kwa kiungo huyo kutoka Kenya mwenye umri wa miaka 20, zimefanya clu nyingi zinazoshiriki ligi kuu ya uingereza kufuatilia kwa ukaribu maendeleo na upatikanaji wa mchezaji huyo huku club kama Liverpool,QPR, Newcastle,West Ham na Stoke City  pia zikitajwa.

Victor Wanyama alinunuliwa mwaka jana na Celtic kutoka timu moja inayojulika kwa jina la  Beerschot   ya nchini Belgium kwa ada ya pound 900,000 (laki tisa) na kufanikiwa kufanya vizuri katika msimu ulipita kwenye ligi ya Scotland, ameshawataarifu timu yake hiyo kuwa ikitokea nafasi ya yeye kutaka kunuliwa na club inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza  wasimbanie kwani yupo tayari kwa hilo.


Ikiwa hili litawezekana basi itakua habarinjema kwa Kenya na Africa mashariki kwa ujumla, hatimae milango ya bahati  na kuangaliwa kwa wachezaji wetu wa soka itafunguka!nadhani si mbali sana kuanzia sasa tutashuhudia wachezaji wetu ndani ya premiership hili linawezekana, tunamtakia kila la kheri Victor Wanyama na kumuombea kufanikisha hilo!

No comments:

Post a Comment